Friday, April 25, 2014

TABIA CHAFU BONGO MOVIE HASA WASANII WA KIKE..STEVE NYERERE AFUNGUKA, DAWA YAO INAKUJA...!

MWENYEKITI wa Bongo Muvi, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amesema kuwa kuna baadhi ya wasanii feki wana tabia chafu zinazoichafua taasisi hiyo, jambo ambalo hawezi kukubaliana nalo.
Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ akisisitiza jambo.

Akipiga stori na paparazi wetu, kiongozi huyo alisema anashangazwa na wasanii hao wengi wao wakiwa wa kike ambao skendo kwao siyo ishu na wamekuwa wakijitambulisha kama wasanii wa Bongo Muvi.

Stive Nyerere.
“Watu wengi wanapenda kujisema wapo Bongo Movie wakati hawatambuliki kabisa kwenye chama chetu, yote hiyo ni sababu ya kutaka kukuza majina kwa kuwa wanaona umoja huu umeshika chati, lazima nitalito-komeze swala hilo, kama mtu anatamani kuwa mwenzetu ni bora ajiunge akiwa msafi na siyo kutuchafua,” alisema Steve.

No comments:

Post a Comment

INAYOFANANA

QWWWWWWWWWWWWWWW

Popular Posts